"WEWE SI WA KAWAIDA, HUPASWI KUISHI
KIKAWAIDA"
Kama ndani yako unatamani kufanya vitu
visivyo vya kawaida tena ambavyo vinalenga kumpa Mungu utukufu, kamwe usikubali
kuishi kama mtu wa kawaida.Ni lazima mfumo wako wa maisha ubadilike na
usifanane na ule wa watu wanaoishi kikawaida kawaida.Ukitamani kufanya mambo ya
siyo ya kawaida kamwe hawezi ukalala kwa jinsi ya kawaida, huwezi ukawaza kwa
jinsi ya kawaida, hata kuamua kwako hakuwezi kuwa kwa kawaida kawaida.Maana
ndani yako wewe si mtu wa kawaida hata kidogo tena umebeba vitu vya kimungu
visivyo vya kawaida.
Watu wa kawaida kazi yao kubwa ni kungojea
mambo ya tokee na kupokea,lakini watu wasio wa kawaida kazi yao kubwa ni kufanya
mambo yatokee.Watu wa namna hii huona mahali ambapo wengine hawawezi kuona,huvuka
mahali ambapo wengine hawawezi kuvuka,hufikiri mambo ambayo wengine wameshindwa
kufikiria.Watu wasio wa kawaida hutafuta kwa bidii na kutoa majibu ya mambo
mbalimbali ambayo yanaikabili jamii inayo wazunguka.
Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya
imara kuitwa kwenu na uteule wenu: maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.
<<2 Petro 1:10>>
“Faith isn’t sitting around waiting for things to happen!” – Dani
Johnson
No comments:
Post a Comment